Friday 16 June 2017

DR. JOHN KHANJI  maembe mabichi kwasababu yakufundishia

DR. JOHN KHANJI     pia tunafundisha ujasiriamali wausindikaji
DR. JOHN KHANJI     watu wanapata vipimo
DR. JOHN KHANJI         nibaadhi ya bidhaa
karibuni
DR. JOHN KHANJI
Tip: Search for English results only. You can specify your search language in Preferences
Mlonge, mlongo, mronge, mrongo, mkimbo au mzunze (Moringa oleifera) ni mti wa jenasi pekee, Moringa, ya familia Moringaceae. Asili ya mti huu ni Uhindi ...

Jitibu magonjwa 300 kwa kutumia Mlonge - fadhilipaulo.com

www.fadhilipaulo.com/jitibu-magonjwa-300-kwa-kutumia-mlonge/
Jul 16, 2016 - Karibu kila sehemu ya mti huu hutumika kama dawa. Majani ya mlonge yanaweza kutafunwa mabichi, yaliyochemshwa kama mboga au ...

Ujue Mmea wa Mlonge na faida zake kwa binadamu | JamiiForums | The ...

https://www.jamiiforums.com › ... › JF Doctor
Dec 5, 2007 - Moringa (Moringa spp.) maarufu kama Mlonge ni miongoni mwa miti muhimu kuliko yote duniani. Mti huu ukuao haraka hupandwa katika ...

Mlonge: Mmea wa maajabu kwenye lishe - IPP Media

m.ippmedia.com/sw/.../mlonge-mmea-wa-maajabu-kwenye-lishe
KAMA kuna mti wenye faida nyingi za kiafya, basi mlonge unaweza kuwa unaongoza. Baadhi ya wataalam wa tiba asilia wanaeleza kuwa kila eneo la mti huu, ...

Jitibu Magonjwa 300 Kwa Kutumia Mti wa Mlonge - Udaku Special Blog

www.udakuspecially.com/.../jitibu-magonjwa-300-kwa-kutumia-mt...
Jul 24, 2016 - Mlonge au moringa oleifera kwa kiingereza umekuwa ukijulikana kama mti wa miujiza kwa karne nyingi katika baadhi ya nchi za Afrika, Asia ...

MLONGE Faida za mti wa Mlonge Mti wa... - Kilimo Na Ufugaji ...

https://www.facebook.com/.../photos/a.../804163863021564/?type...
MLONGE Faida za mti wa Mlonge Mti wa Mlonge una faida nyingi ambazo hazifahamiki kwa watu wengi. Faida za mti huu zinatokana na sehemu mbalimbali za ...

Mlonge Leaf Powder - Medical & Health | Facebook

https://www.facebook.com › Places › Tanga, Tanzania › Medical & Health
Rating: 4.7 - ‎6 votes
Mlonge Leaf Powder. 368 likes · 4 talking about this · 136 were here. A Powder made from dried leaves of the Mlonge Tree (Moringa Oleifera). The powder...

UTAFITI UNAONESHA MMEA AINA YA MLONGE NI MBOGALISHE ...

www.suanet.ac.tz/.../62-utafiti-unaonesha-mmea-aina-ya-mlonge-ni...
Profesa Msuya amesema kuwa “imethibitishwa na kufanyiwa utafiti kupitia Idara yetu hii ya Sayansi na Chakula
DR. JOHN KHANJI
Tip: Search for English results only. You can specify your search language in Preferences
Mlonge, mlongo, mronge, mrongo, mkimbo au mzunze (Moringa oleifera) ni mti wa jenasi pekee, Moringa, ya familia Moringaceae. Asili ya mti huu ni Uhindi ...

Jitibu magonjwa 300 kwa kutumia Mlonge - fadhilipaulo.com

www.fadhilipaulo.com/jitibu-magonjwa-300-kwa-kutumia-mlonge/
Jul 16, 2016 - Karibu kila sehemu ya mti huu hutumika kama dawa. Majani ya mlonge yanaweza kutafunwa mabichi, yaliyochemshwa kama mboga au ...

Ujue Mmea wa Mlonge na faida zake kwa binadamu | JamiiForums | The ...

https://www.jamiiforums.com › ... › JF Doctor
Dec 5, 2007 - Moringa (Moringa spp.) maarufu kama Mlonge ni miongoni mwa miti muhimu kuliko yote duniani. Mti huu ukuao haraka hupandwa katika ...

Mlonge: Mmea wa maajabu kwenye lishe - IPP Media

m.ippmedia.com/sw/.../mlonge-mmea-wa-maajabu-kwenye-lishe
KAMA kuna mti wenye faida nyingi za kiafya, basi mlonge unaweza kuwa unaongoza. Baadhi ya wataalam wa tiba asilia wanaeleza kuwa kila eneo la mti huu, ...

Jitibu Magonjwa 300 Kwa Kutumia Mti wa Mlonge - Udaku Special Blog

www.udakuspecially.com/.../jitibu-magonjwa-300-kwa-kutumia-mt...
Jul 24, 2016 - Mlonge au moringa oleifera kwa kiingereza umekuwa ukijulikana kama mti wa miujiza kwa karne nyingi katika baadhi ya nchi za Afrika, Asia ...

MLONGE Faida za mti wa Mlonge Mti wa... - Kilimo Na Ufugaji ...

https://www.facebook.com/.../photos/a.../804163863021564/?type...
MLONGE Faida za mti wa Mlonge Mti wa Mlonge una faida nyingi ambazo hazifahamiki kwa watu wengi. Faida za mti huu zinatokana na sehemu mbalimbali za ...

Mlonge Leaf Powder - Medical & Health | Facebook

https://www.facebook.com › Places › Tanga, Tanzania › Medical & Health
Rating: 4.7 - ‎6 votes
Mlonge Leaf Powder. 368 likes · 4 talking about this · 136 were here. A Powder made from dried leaves of the Mlonge Tree (Moringa Oleifera). The powder...

UTAFITI UNAONESHA MMEA AINA YA MLONGE NI MBOGALISHE ...

www.suanet.ac.tz/.../62-utafiti-unaonesha-mmea-aina-ya-mlonge-ni...
Profesa Msuya amesema kuwa “imethibitishwa na kufanyiwa utafiti kupitia Idara yetu hii ya Sayansi na Chakula
DR. JOHN KHANJI

Sunday 16 April 2017

hata hivyo ukweli ni kwamba tende hazitakiwa kutumiwa katika kipindi cha mfungo pekee, bali inatakiwa kila wakati walau mara mbili kwa wiki mtu aweze kutumia tende. Na zifuatazo ndizo faida za matumizi ya tende. 1. Ukila tende mara kwa mara, mwili wako utapata aina mbalimbali za madini na vitamin za kutosha, ambazo zinapatikana kwenye tunda hili maarufu duniani. Katika tende kuna kiasi kidogo tu cha mafuta (fat). Mafuta haya husaidia kutia joto na nguvu katila mwili wa binadamu. 2. Ulaji wa tende huimarisha na kuboresha mfumo wa usagaji chakula tumboni, hivyo utaondokana na matatizo ya ukosefu wa choo, au matatizo ya kupata choo kigumu kinachosababisha maumivu wakati wa kujisaidia. Pia ndani ya tende kuna virutubisho vya ‘amino acids’ ambavyo ni muhimu mwilini. 3. Ukila tende, mwili utapata nguvu na kukuondolea uchovu ndani ya nusu saa tu, kwa sababu tende ina virutubisho vya sukari asilia kama vile ‘glucose’, ‘sucrose’ na ‘fructose’. Ili kupata faida zaidi za tende, changanya na maziwa fresh kisha kula. Unapojisikia mchovu, badala ya kunywa vinywaji baridi vinavyodai kuongeza nguvu, kula tende, hata kiasi cha punje tatu kinatosha. Kwa wafunga saumu, ndiyo maana inashauriwa kuanza kufungua kwa kula tende ili kuurejeshea mwili wako nguvu iliyopotea siku nzima. 4. Tende ina madini pia aina ya ‘potassium’ na kiasi kidogo cha chumvi (sodium). Madini haya husaidia uimarishaji wa mishipa ya fahamu. Watafiti wamegundua kwamba ulaji kiasi wa ‘potassium’ huweza kumuepusha mtu na kupatwa na kiharusi (stroke). Pia tende husaidia kupunguza lehemu (cholesterol) mwilini (LDL Cholesterol). 5. Kwa wale wenye matatizo ya ugonjwa wa kukauka damu mwilini (anemia), wanaweza kupata ahueni kwa kula tende kwa wingi ambayo ina kiwango cha kutosha cha madini ya chuma ambayo huhitajika katika utengenezaji wa damu mwilini. Wakati vitu vitamu vingine huozesha meno, utamu wa tende huzuia uozaji wa meno. Hizo ni baadhi ya faida chache kati nyingi zinazomsaidia mtu katika ku

Monday 3 April 2017

NURU

Ni dawa inayotibu macho yanayowasha,kuuma na kupoteza nuru ya kuuona pia kushindwa kusoma vizuri na kutoa machozi




NA DK.JOHN KANJE

HAKIKA NA KWELI

DR. JOHN KHANJI
Ni dawa inayoondoa mafuta machafu katika mishipa ambayo yanasababisha presha kwa hiyo ni dawa inayotibu presha na huondoa uric acid katka mwili gesi katika tumbo na maumivu ya kiuno na mgongo

KOMAA

Ni dawa ya kutibu meno yaliyotoboka ,fizi kutoa damu na kuwasha,meno yanayotoboka,meno yanayokufa ganzi ukinywa maji baridi au moto na kinywa kutoa harufu mbaya
DR. JOHN KHANJI

FURAHA

DR. JOHN KANJE
Ni  Dawa ya kutibu tatizo la fangasi sehemu za siri pia huondoa harufu mbaya hufanya sehemu kuwa na hali nzurisana na mishipa kuwa mizuri inafanya sehemu hiyo kuwa ndogo vizuri huondoa majimaji meupe yanyotoka sehemu kama hiyo
Matumizi; nawia kifuniko kimoja asubuhi na jioni

Friday 24 March 2017

BAADHI YA DAWA

DR. JOHN KHANJ      NI DAWA  MBALI MBALI ZA KUTIBU MAGONJWA KARIBUNI SANA

Wednesday 22 March 2017

usoni MUUNGWANA BLOG / 13 hours ago  Chunusi ni ugonjwa wa ngozi ambao hujit-okeza kama viuvimbe/vipele vidogo vidogo hasa sehemu za uso,kifuani na hata mgongoni.Vipele hivi hutokea wakati vishimo vya kupitisha jasho katika ngozi vinapozibwa kwa mafuta au seli za ngozi zilizokufa au wadudu yaani Bacteria. Kwa lugha ya kidaktari chunusi huitwa Acne Vulgaris.Chunusi ndio ugonjwa wa ngozi ambao humwathiri binadamu kwa kiasi kikubwa kwa mfano nchini Marekani pekee huathiri watu zaidi ya milioni kumi na sa-ba..Chunusi huweza kujitokeza katika umri wowote lakini huathiri sana vijana hasa wa-kati wa balehe (adolescents) . Karibu asilimia 85 ya vijana kati ya umri wa miaka 12 hadi 25 hupata chunusi na zaidi ya asilimia 20 ya wanawake wenye umri wa zaidi ya miaka ishirini hupata chunusi wakati mwingine hata watoto wadogo pia huweza kupata chunusi hii ni tofauti na watu wengi wanavyofikiria kuwa chunusi ni dalili ya balehe. Chunusi ni ugonjwa unaoathiri vifuko au glandi za ngozi.Katika ngozi ya binadamu kuna glandi ziitwazo Sebaceous ambazo zipo chini ya ngozi na kazi yake kubwa ni kutoa mafutamafuta yaitwayo Sebum ambayo hu-saidia kuiweka ngozi kuwa nyevu na yenye mvuto. Wakati wa balehe mwili wa binadamu hutoa Sebum kwa wingi na kwa sababu wakati huu vikemikali vya mwili yaani sex hormones hutolewa kwa wingi hasa hormone ya kiume iitwayo androgen husababisha utoaji wa sebum kuwa mwingi zaidi kuliko kawaida. Sebum inapotolewa kwa wingi huungana na seli za ngozi zilizo-kufa na kutengeneza mchanganyiko mzito kama nta uitwao comedo ambao huziba vishimo vya kutolea joto. Maambukizi zaidi hutokea pale ambapo vijidudu yaani baktaria vinaposhambulia vishimo vilivyoziba hapo kivimbe ambacho watu wengine huita Pimple hujitokeza pale ambapo Sebum, bacteria, seli za ngozi na seli nyeupe za damu zinapo-changanyika na kujikusanya katika vishimo vya jasho vilivyoziba na eneo husika hupata vivimbe au vipele ambavyo tunaviita chunusi. Ukubwa wa kipele hutegemea ngozi ya mtu au kiasi cha mchanganyiko nilioeleza hapo juu katika eneo husika.Vipele vinaweza kuwa vidogo au vikubwa. Chunusi wakati mwingine husababisha mabaka katika ngozi hali hii hutokea pale ambapo seli za ngozi zilizoharibika huondolewa na seli mpya kutengenezwa. Ngozi mpya hutengenezwa kirahisi tu mahali palipokuwa na chunusi hali hii husababisha mlingano usiosahihi wa ngozi na hutoa kidonda ambacho baadaye hubaki kama baka. Chunusi hutokea zaidi katika uso,kifua ,mabega na mgongoni kwa sababu maeneo hayo yana vifuko au glandi za Sebaceous nyingi. CHANZO CHA CHUNUSI Chanzo halisi cha chunusi hakijulikani.hata hivyo baadhi ya vitu vinavyoongeza uwezekanifu wa kupata chunusi ni; UMRI – Kama nilivyosema hor-mone/vikemikali hutolewa kwa wingi sana mtu anapofikia umri wa kubale-he.Kemikali hizi huongeza utengenezaji wa nta (sebum) katika ngozi ambayo huchochea kutokea kwa chunusi VIPODOZI –Baadhi ya vipodozi kama Make-up za kina dada na Sprays za ny-wele zina mafuta ambayo yanaweza kusababisha chunusi kuwa nyingi zaidi. CHAKULA- Chunusi hazisababishwi na chakula bali baadhi ya vyakula hufan-ya chunusi kuwa nyingi zaidi. DAWA-Chunusi zinaweza kujitokeza kutokana na kutumia dawa kadhaa kama vile antibiotics,Vidonge vya uzazi wa mpango,steroids na tranquilizers.Steroid ni dawa zenye homoni zilizotengenezwa kitaalamu ambazo wakati mwingine wanariadha huzitumia tofauti na ma-kusudio ili kuongeza unene wa misuli yao. MAGONJWA- Magonjwa yatokanayo na matatizo katika vikemikali (hormonal disorders) huongeza matatizo ya chunusi hasa kwa wasichana. MAZINGIRA- Chunusi huweza kuwa nyingi zaidi hasa unapoishi mazingira yenye mafuta,grisi au hewa chafu .Kutoa jasho sana hasa katika mazingira ya joto huongeza uwezekanifu wa kupata chunusi. JINSIA-Wavulana hupata sana chunusi kuliko wasichana. FAMILIA- Wakati mwingine chunusi hujitokeza sana kwa wanafamilia wa familia kadhaa kuliko nyingine. HOMONI- Mabadiliko ya homoni za mwili hasa wakati mwanamke akiwa katika siku zake,ujauzito au mwanamke anapokuwa na umri mkuwa hupelekea kupata chunusi. USAFI WA MWILI- Kutumia sabuni zenye kemikali,kujisugua sana na kuzitoboatoboa chunusi au vipele hu-sababisha chunusi kuongezeka zaidi.Kukaa muda mrefu na jasho mwi-lini au kutooga huongeza uwezekanifu wa kupata chunusi MAWAZO AU STRESS-Mtu anapokuwa na mawazo mengi vimkemikali kadha hutolewa mwilini ambavyo huwe-za kuchangia au kusababisha chunusi DALILI ZA CHUNUSI Vipele au vivimbe vidogo vidogo ambavyo pengine husababisha mwasho au vinavyouma ni dalili ya chunusi.Wakati mwingine huweza kujitokeza kama baka dogo na wakati mwingine mtu anaweza utambuzi wa chunusi unaweza kuwa mgumu kutokana na watu walivyomakini au wanavyojenga wasiwasi kubwa katika mwonekano wao hasa usoni.Ikumbukwe kuwa kutokana mwonekano wa chunusi ni rahisi sana. Daktari kuzigundua, japokuwa katika familia zetu ni mara chache sana mtu akaenda kumwona daktari au mtaalamu wa magonjwa ya ngozi kwa sababu ya chunusi.Pale inavyotokea hivyo basi hali inakuwa ni mbaya zaidi.Hata hivyo si vibaya kumwona daktari ambaye atakuuliza kuhusu chakula, ngozi, dawa unazotumia na vitu vingine vinavyowe-za.kuchangia mtu kupata chunusi MATIBABU Matibabu ya chunusi yanajumuisha kupunguza utoaji wa anta (sebamu ), kuondoa seli za ngozi zilizokufa na kuua wadudu yaani bacteria. Matibabu huweza kutofautiana kutokana na wingia au ukubwa wa tatizo. Suala la kuzingatia ni kuepuka mambo yanayoweza kusababisha chunusi kama nilivyoeleza hapo juu. DAWA ZA KUPAKA Kuna dawa za kupaka ambazo hupaka katika eneo la ngozi lililoathirika kwa chunusi. Dawa hizi hupatikana kama cream,lotion,gel au pad. Dawa hizi hutumika kutibu chunusi ambazo haziko katika hali mbaya hasa kama kuna vijipele vidogo vidogo tu. Mojawapo ya dawa hizi ni antibi-otic kama zenye mchanganyiko wa gentamyicin na betamethasone au dexame-thasone kama vile Gentrisone au Gentriderm cream, Erythromycin,B-Tex na kadhalika.Pia Persol forte Gel husaidia hasa ukianza na asilimia ndogo (2.5%) na kuen-delea kadri ngozi yako inavyohimili dawa. Gentamycin huua wadudu wanaosababisha chunusi wakati dawa nyingine huondoa mwasho. Dawa nyingine ni zile zinzolainisha nta au Comedolytics na kufanya vishimo vya jasho kufunguka na dawa nyingine huongeza kasi ya utengenezwaji wa seli mpya za ngozi. Dawa hizi za kupaka hushauriwa kupakwa angalau mara mbili au tatu kila siku hasa baada ya kusafisha kwa maji safi na sabuni ya kawaida na kukausha kwa taulo eneo lenye chunusi na matibabu yanaweza kuchukua wiki kadhaa. DAWAZA KUMEZA Wakati mwingine daktari anaweza kumshauri mgonjwa kutumia dawa za kumeza kulingana na wingi au ukubwa wa tatizo. Dawa kama antibiotics huua wadudu na huzuia chunusi ,dawa hizo ni kama vile Erythromycin topical, Accutane (isotret-inoin), Benzamycin Cleocin T (clindamycin phosphate), Desquam-E (benzoyl peroxide) Minocin (minocycline hydrochloride) na ”Si vema kujinunulia mwenyewe tu na kuanza kutumia bila ushauri wa daktari au mtaal-amu wa magonjwa ya ngozi.” Wanawake wenye chunusi zisizotibika wanaweza kupewa Anti-androgens kama vile baadhi ya vidonge wa uzazi wa mpango.Chunusi sugu hutibiwa kwa ciorticosteroids na anti-iflammatory drugs ambazo hutibu chunusi sugu ambazo huitwa Acne fulminans na hupatikana zaidi kwa vijana. MATIBABU MENGINE Kwa nchi zilizoendelea matibabu yanaweza kuwa hata upasuaji mdogo (skin grafting) au plastic surgery kama chunusi imesaba-bisha baka kubwa na kuna njia kama vile Chemical peel ambapo kemikali hupakwa kwenye ngozi na inapokauka kipande au gamba la juu la ngozi huondolewa na kuondoa baka. MATIBABU MBADALA Haya hujumuisha lishe bora na usafi wa mwili.Ni vema kuoga mara kwa mara na kujifuta maji kwa taulo safi na kuiweka ngozi katika hali ya ukavu nakuepuka upakaji wa mafuta mengi ya mgando hasa wakati wa joto. Watu wenye chunusi wanashauriwa kulAa mlo kamili wenye vyakula vyenye madini ya zinki,nyuzinyuzi, matunda, mboga za ma-jani,vitamin B complex na Chromium. Ni vema kuepuka au kupunguza matumizi ya pombe,vyakula vya maziwa, tumbaku, sukari, vyakula vilivyoandaliwa viwandani na vyakula vyenye Iodine nyingi kama vile chumvi MUHIMU Chunusi haziwezi kutibika kabisa japokuwa iwapo matibabu Yatakuwa sahihi watu 60 kati ya 100 hupona na unapokuwa unatumia dawa usitarajie kupona haraka kwani inaweza kuchukua hata miezi miwili kupata nafuu na zinaweza kujitokeza unapoacha kutumia dawa.Chunusi pia huweza kupona kwa kuacha mabaka ambayo kwa hapa nchini hakuna utaalamu sahihi wa kuyaondoa bali huweza kuondoka kadri muda unavyoenda au kwa kemikali kali ambazo zinaweza kuwa na madhara katika ngozi. MAMBO YA KUFANYA ILI USIPATE CHUNUSI Hakuna njia sahihi ya kujizuia ila unaweza kufanya yafuatayo; Osha taratibu sehemu unayodhani ina chunusi kwa maji safi na sabuni angalau mara mbili kila siku huku ukisugua taratibu ,usikwaruze kwa kucha au kitu choichote kigumu. Tumia make-up au vilainisha ngozi visivyo na mafuta mgando Osha nywele zako kila mara na epuka nywele kuziba uso (kwa wenye nywele ndefu) Kula mlo kamili na epuka vyakula vyenye mafuta mengi. Usibinye au kutoboa vipele kwa pini au kitu chenye ncha kali. Epuka kukaa sana juani,mwanga wa asubuhi ni mzuri ili kupata vitamin D Punguza mawazo

Friday 3 March 2017

Jinsi ya utengenezaji wa dawa

namna yauandaaaji dawa ya vidonda vyatumbo
>majani 12 ya mpapai
>kitunguu swaum kimoja
>mziwaziwa majani kiganja kiwe kimejaaa
brendi katika kisagio changanya namaji ilibaada ya kusanga itoke juice lita 1na nusu tumiaa nusulita kila baada ya masaa 6 tumia kwa wiki tatu mfulilizo

Monday 27 February 2017

DAWA YA AMINI

AMINI
Ni dawa ya mitishamba asilia inayotibu tatizo la aleji na kuondoa aleji katika damu. Kutibu mwili kuwasha, Aleji ya vumbi na kujikuna mara kwa mara, Aleji ya baridi, Aleji  ya manukato
Inatengenezwa na kuandaliwa na
 KANGAA HERBAL CLINIC.
P.O.BOX  1719 Moshi.
Mob: 0766 807 205
           0764 302 904
           0754 240 211
E-mail
:kangaaherbalclinic@gmail.com

HUDUMA ZETU ZIPO POPOTE ULIPO KWA MAWASILIANO HAPO JUU.

DAWA YA KIRUMARUMA

KIRUMARUMA

Ni dawa ya kutibu tumbo linalouma, amweba, taifodi, kutokwenda choo na nyongo. Huondoa mafuta machafu tumboni na uzito unazozidi (tumia kijiko kimoja kikubwa  1*2)
change la nguri kwa wanaume, kinamama na kupunguza kitambi

NB:
Haruhusiwi kutumia mama mjamzito.
Inatengenezwa na kuandaliwa na
 KANGAA HERBAL CLINIC.
P.O.BOX  1719 Moshi.
Mob: 0766 807 205
           0764 302 904
           0754 240 211
E-mail :kangaaherbalclinic@gmail.com

HUDUMA ZETU ZIPO POPOTE ULIPO KWA MAWASILIANO HAPO JUU.

MAFUTA YA QUEEN ONE

QUEEN ONE

Natural Hair Food.

Mafuta ya nywele ya asili ambayo yanakuza nywele kwa haraka. Hufanya nywele kua nyeusi na hufanya nywele zisikatike pia huondoa mawasho.

INGREDIENTS.
Vegetable, Alovera, Avacardo, Casrol
Oil, Olive, Honey, Bamboo Oil

Inatengenezwa na kuandaliwa na

 KANGAA HERBAL CLINIC.
P.O.BOX  1719 Moshi.
Mob: 0766 807 205
           0764 302 904
           0754 240 211
E-mail :kangaaherbalclinic@gmail.com

HUDUMA ZETU ZIPO POPOTE ULIPO KWA MAWASILIANO HAPO JUU.

DAWA YA BINGWA

BINGWA

Dawa ya asili inayotibu miguu, kuvimba mwili, kuchoka miguu,  kuwaka moto.
Ganzi,  vichomi,  uti wa mgongo, kusagika kwa mifupa na magoti
kushindwa kuchuchumaa.

MATUMIZI:
Tumia katika maji ya moto kijiko kikubwa  (1*2)
Inatengenezwa na kuandaliwa na
 KANGAA HERBAL CLINIC.
P.O.BOX  1719 Moshi.
Mob: 0766 807 205
           0764 302 904
           0754 240 211
E-mail :kangaaherbalclinic@gmail.com

HUDUMA ZETU ZIPO POPOTE ULIPO KWA MAWASILIANO HAPO JUU.

DAWA YA AMBA

AMBA

Ni dawa ya kutibu mtu mwenyesukari ya kupanda na kushuka
husaidia kongosho kupata nguvu ya kuchuja vizuri pia huondoa uric aside katika viungo na husaidia mifupa inayosagika na kuvimba

MATUMIZI:
Tumia mifuniko mitatu kila baada ya masaa sita (3*3)

Inatengenezwa na kuandaliwa na

 KANGAA HERBAL CLINIC.
P.O.BOX  1719 Moshi.
Mob: 0766 807 205
           0764 302 904
           0754 240 211
E-mail :kangaaherbalclinic@gmail.com

HUDUMA ZETU ZIPO POPOTE ULIPO KWA MAWASILIANO HAPO JUU.

DAWA YA TAYARI

TAYARI

Ni dawa ya kutibu malaria na taifodi sugu

MATUMIZI:
Tumia mifuniko minne (4*2)
Inatengenezwa na kuandaliwa na
 KANGAA HERBAL CLINIC.
P.O.BOX  1719 MoShi.
Mob: 0766 807 205
           0764 302 904
           0754 240 211
E-mail :kangaaherbalclinic@gmail.com

HUDUMA ZETU ZIPO POPOTE ULIPO KWA MAWASILIANO HAPO JUU.


DAWA YA SONGOTA

SONGOTA

Ni dawa ya kutibu U.T.I  tumbo kuuma chini ya kitovu mngurumo
kuwasha sehemu za haja ndogo

MATUMIZI:
Tumia mifuko minne (4*2)
Inatengenezwa na kuandaliwa na
 KANGAA HERBAL CLINIC.
P.O.BOX  1719 Moshi.
Mob: 0766 807 205
           0764 302 904
           0754 240 211
E-mail :kangaaherbalclinic@gmail.com

HUDUMA ZETU ZIPO POPOTE ULIPO KWA MAWASILIANO HAPO JUU.

DAWA YA SAFISHA

SAFISHA

Ni maji ya kunywa kabla ya kunywa dawa yeyote ili kuufanya mwili
kupokea dawa. Hutoa sumu haraka, kuondoa mafuta machafu na kulainisha uchafu katika tumbo hufungua mishipa yote ya mwili na kuipa nguvu wakati wa kunyanyuka, paralaizi,huandaa mwili kupokea dawa na kupata hamu ya kula chakula na maji.

MATUMIZI:
Tumia mifuko mitatu kila baada ya masaa sita (3*3)
Inatengenezwa na kuandaliwa na
 KANGAA HERBAL CLINIC.
P.O.BOX  1719 Moshi.
Mob: 0766 807 205
           0764 302 904
           0754 240 211
E-mail :kangaaherbalclinic@gmail.com

HUDUMA ZETU ZIPO POPOTE ULIPO KWA MAWASILIANO HAPO JUU.

DAWA YA MZACHA


MZACHA:


Ni dawa ya asili yenye mchanganyiko wa miti na mimea zaid ya 60.
HUTIBU MAGONJWA YAFUATAYO.
.Kuosha suumu mwilini
.Baridi ya bisi
.Miguu kuwaka moto
.Fangasi ya kizazi
.Malaria sugu,kifua,figo,wegu taifod
.Mifupa kuwa na ganzi
.Amweba
.Presha
.Kuumwa mgongo,kiuno na magoti
.Kuosha mirija ya mkojo
.Aleji
.Tambazi
.Tumbo kuunguruma
.Kizunguzungu
Inatengenezwa na kuandaliwa na
 KANGAA HERBAL CLINIC.
P.O.BOX  1719 Moshi.
Mob: 0766 807 205
           0764 302 904
           0754 240 211
E-mail :kangaaherbalclinic@gmail.com

HUDUMA ZETU ZIPO POPOTE ULIPO KWA MAWASILIANO HAPO JUU.

Saturday 25 February 2017

FAIDA ZA ALOE VERA

Mshubiri ni mmea wenye Miujiza ya kutibu maradhi sugu kama ugonjwa wa Saratani (Cancer), ugonjwa wa Kisukari, kolesto, ugonjwa wa kuvimba sehemu ya mwili na magonjwa mengine mengi.

Faida za mmea wa aloe vera au mshubiri

1. Huondoa uvimbe katika jicho
Weka kiasi kidogo cha majimaji ya mu-aloe vera freshi kisha kuamka asubuhi, acha kwa dakika kadhaa kisha jisafishe. Uvimbe lazima ukimbie. Pia unaweza kuloweka pamba katika majimaji ya mualoe vera na kisha jisafishe katika jicho lenye uvimbe.
2. Huzuia na kuondoa michirizi ya tumbo itokanayo na ujauzito
Anza kwa kupakaa majimaji ya mualoevera juu ya tumbo lako na ufanye kama masaji hivi taratibu juu ya tumbo mara 2 kwa siku katika kipindi chote cha ujauzito na baada ya kujifungua kwa miezi michache mpaka michirizi ipotee yote.
3. Hutibu bawasiri
Ile ile sifa moja iliyonayo ya kutibu uvimbe ambayo inaweza pia kutibu malengelenge na uvimbeuchungu kwenye mwako wa mwili, ndiyo hiyo hiyo pia husaidia kutibu au kupunguza maumivu ya bawasiri. Chana tawi la aloe vera freshi na upate jeli yake, kisha pakaa eneo linalosumbuliwa na bawasiri mara mbili mpaka tatu kwa siku kwa wiki kadhaa hasa kama bawasiri imejitokeza sehemu ya nje hadi hapo uvimbe huo utakapopotea.
4. Ni tiba kwa matatizo ya tumbo
Kama utainywa, hutibu vidonda vya tumbo na kiungulia, na kwa ujumla ni kuwa husafisha mfumo wote wa mmeng’enyo wa chakula. Chukua jeli ya aloe vera nusu kikombe (ml 125) changanya na maji ya kawaida nusu kikombe tena kupata ujazo wa  robo lita, changanya vizuri mchanganyiko huu na unywe kutwa mara 2 kwa siku 3 hadi wiki 1 kujitibu matatizo ya tumbo kama kuum, kuondoa sumu, kuunguruma, kuhara na hata kutibu malaria.
Madhara ambayo yameripotiwa kutokana na kunywa aloe vera ikiwa freshi ndani ya tumbo ni pamoja na kuharisha na matatizo kwenye figo.
5. Huziimarisha kucha dhaifu
Kwa taratibu pakaa majimaji ya aloe vera juu ya kucha zako sehemu zote juu na chini kila siku na uzitazame baada ya siku kadhaa uone zitakavyokuwa zimerudisha ule uzuri na ugumu wake wa mwanzo.
6. Huondoa Makeup
Kwa usalama kabisa huondoa makeup kwenye jicho na ni nzuri kwa ngozi laini inayozunguka jicho lako.
7. Husafisha ngozi na kuondoa alama zitokanazo na kuungua na jua
Chunusi, ukurutu na kuungua kwa ngozi kutokana na jua vyote hivi vinatibika kirahisi kwa kutumia aloe-vera. Pakaa mara 2 hadi 3 kwa siku katika ngozi mpaka uone umepona kabisa. Mu-aloe vera pia una sifa ya kupoza kama ilivyo menthol ambayo unaufanya Mu-aloe vera kuwa dawa ya asili nzuri zaidi katika kutibu alama zitokanazo na kuungua na jua.
8. Ni jeli ya asili ya kunyolea na baada ya kunyoa
Aloe Vera ni dawa ya asili katika kutibu michubuko asante kwa vimeng’enya vyake ambavyo huwa na kiasi kingi cha maji ambayo ni mhimu kuzuia kukauka kwa ngozi. Wakati unanyoa ndevu pakaa jeli ya aloe vera na hata baada ya kunyoa pakaa kama after shave jel kuzuia na kuponya michubuko itokanayo na kunyoa.
9. Huondoa makunyanzi na mikunjo ya ngozi
Ngozi hupenda sana Vitamini C na E ambazo zote zinapatikana katika aloe vera na kusaidia kuboresha unene wa ngozi na kuiacha katika hali ya umajimaji. Ikiwa utachanganya jeli ya aloe-vera na mafuta ya asili ya nazi utapata krimu nzuri ya kuongezea viinilishe, mafuta mhimu na unyevunyevu katika ngozi.
Jeli ya Aloe Vera hupenyeza katika ngozi kwa haraka mara nne zaidi ya maji ya kawaida na sifa yake ya kulainisha ngozi husaidia ngozi kubaki na unyevunyevu muda wote.
10. Hutibu homa na mafua
Jeli ya Aloe Vera huongeza kinga ya mwili. Mu-aloe-vera una viinilishe vingi sana mhimu kwa afya ya binadamu. Ina Vitamini A, B, C, na E. Mmea huu una orodha ndefu ya madini mhimu kwa mwili na vimeng’enya vingine mhimu.
11. Vitamini B12 kwa wale wasiotumia nyama (Vegans)
Matumizi makuu ya aloe vera kimatibabu ni kusaidia na kuboresha uundwaji wa bakteria wazuri. Kwa kuongezea aloe vera huwa na jumla ya madini ambayo bakteria huyahitaji katika kutengeneza Vitamini B12.
12. Huongeza nguvu mwilini
Matumizi mengine ya kitabibu ya mmea wa mu aloe vera au mshubiri kwa kiswahili chake hasa, ni kuongeza usawa wa nguvu mwilini. Hii ni kutokana na uwepo wa vitamin b 14 na viinilishe vingine ambavyo husaidia kubadili asilimia kubwa ya chakula katika tumbo lako na kuunda nguvu.
13. Huondoa mba kichwani
Changanya jeli ya asili ya aloe vera na shampoo yako, dakika chache kabla ya kwenda kulala pakaa vizuri mchanganyiko huo kwenye nywele zako na uache zikauke kidogo na usafishe nywele zako asubuhi.
14. Huondoa maumivu wakati wa hedhi
Changanya jeli ya Aloe vera na pilipili manga ya unga kidooogo, meza kijiko cha chakula kimoja mara tatu kwa siku kila siku hadi maumivu yatakapoacha.
15. Hulainisha nywele
Jeli ya Aloe vera ni nzuri katika kutibu tatizo la nywele kujisokota na ni mbadala mzuri kwa bidhaa nyingi za madukani zenye gharama kwa ajili ya nywele.
16. Ni dawa ya asili ya kusafishia mdomo
Changanya jeli ya aloe-vera ml 100, vijiko 3 vya chai vya baking soda, maji ml 100 na kijiko 1 kidogo cha juisi ya limao. Changanya vizuri vyote kwa pamoja na utumie kama dawa yako ya asili ya kusafishia mdomo.
17. Hutibu matatizo katika mmeng’enyo wa chakula
Juisi ya Aloe vera ni nzuri sana katika kurekebisha matatizo katika mmeng’enyo wa chakula, hurekebisha kuvurugika kwa tumbo na kiungulia. Itumie kama ilivyoelezewa kwenye kutibu matatizo ya tumbo hapo juu namba 4.
18. Hushusha lehemu (Cholesterol)
Tafiti zimeonyesha kuwa kunywa juisi ya aloe vera kwa kipindi kirefu kunaweza kushusha kiwango cha lehemu mwilini. Itumie kama ilivyoelezewa kwenye kutibu matatizo ya tumbo hapo juu namba 4.
19. Hutibu chunusi
Aloe Vera huondoa chunusi kwa kuziondoa seli zilizokufa katika ngozi na hivyo kuvifungua vishimo katika ngozi na kuondoa mafuta yaliyoganda katika hivyo vishimo. Pakaa jeli ya aloe vera moja kwa moja katika eneo lililoathirika na chunusi. Pia makovu yaliyoachwa kutokana na chunusi yanaweza kuondolewa kwa kupakaa jeli ya aloe vera pekee.
20. Hutibu ukurutu na upele
Ukurutu ambao ni matokeo ya juu ya tetekuwanga kwa kawaida hutokea kwa watu wazima wenye kinga ya mwili pungufu. Aloe Vera inaweza kutumika kutibu tetekuwanga zinazosababishwa na kirusi aina ya herpes virus. Kwa kupakaa jeli ya aloe vera moja kwa moja kwenye sehemu zilizowazi hutanua mishipa ya damu jambo linalosaidia kutibu vidonda.
21. Huzuia ngozi kuunguzwa na jua (Sunscreen)
Kupakaa jeli ya Aloe Vera katika mwili hulinda ngozi dhidi ya miale yote ya jua kutua moja kwa moja kwenye ngozi na hivyo kukufanya usizeeke mapema, pia ni dawa nzuri kwa ngozi inayofubaa.
22. Hulainisha sehemu kavu za siri
Aloe Vera hufanya kazi kama kilainishi bora kabisa cha asili katika maeneo ya siri kwa jinsia zote mbili na kutoa unyevunyevu wa asili.
23. Hutibu vidonda katika mdomo
Mu Aloe vera unazo vitamini na asidi amino ambazo husaidia kuzitengeneza upya tishu zilizoharibika. Tafiti zimeonyesha kuwa watu wanaosumbuliwa na vidonda mdomoni waliotumia jeli ya aloe vera walifanikiwa kutibu karibu asilimia 50 haraka zaidi kuliko wale ambao hawakutumia jeli ya aloe vera.
24. Hutibu maambukizi katika uke
Unaweza kutibu maambukizi katika uke kwa kupakaa jeli ya aloe vera kwa nje na kwa kuinywa jeli kupata faida yake ya kutibu fangasi. Mililita 120 mpaka 200 za jeli ya aloe vera kila siku zinaweza kusaidia kutibu maambukizi na fangasi katika mwili na ikiwa utaendelea kuinywa kwa muda mrefu kunaweza kuzuia maambukizi zaidi kutokujirudia baadaye.
25. Husaidia kukaza uke
Wakati sisi wanaume tukilaumiwa kuwa na vibamia, wanawake nao huwa wanapatwa na tatizo la kuwa na uke mkubwa kiasi kwamba unaweza kuhoji huu ni uwanja wa taifa au!. Basi kina mama msiache kunipa zawadi kwa hili. Ikiwa misuli ya uke wako imelegea na uke umekuwa mkubwa na unahitaji kuubana na kuwa mdogo tena basi unachohitaji ni mshubiri freshi. Chukua aloe vera fresh, chukua jeli yake (maji maji yake) na upakae huko ndani kutwa mara 2 mpaka 3 kwa wiki 3 mpaka mwezi mmoja hivi utaona umekuwa kama binti mdogo tena na mme atabaki na wewe. Kazi ni kwenu.
26. Husaidia wawindaji
Wawindaji wa wanyama katika barani Afrika mara kwa mara hupakaa jeli ya aloe vera katika miili ili kupunguza kutokwa jasho na kuondoa harufu yao ya asili katika mwili isisikike na wanyama.
27. Suluhisho kwa watafuna kucha
Burashi kucha za mtoto anayependa kutafuna kucha na jeli ya aloe vera, ile radha ya uchungu katika aloe vera kutamfanya aache kuzitafuna kucha zake.
28. Hutumika katika kupunguza uzito
Watafiti wameweza kugundua kuwa kunywa juisi ya aloe vera husaidia kupunguza sukari kwenye damu jambo mhimu kwa wale wenye kisukari cha aina ya pili. Wanasayansi wanaamini kuwa kuweka kiwango cha sukari chini hupunguza uzito.
29. Hutibu upungufu wa damu (Anemia)
Kunywa jeli ya aloe vera kunasaidia uzalishaji zaidi wa seli nyekundu za damu katika mwili wako na hivyo kutibu tatizo la kupungua kwa damu.
30. Huondoa maumivu ya mishipa
Kutokana na sifa yake ya kutibu uvimbe, unaweza kutibu uvimbechungu (inflammation) katika maungio yanayopelekea maumivu katika mishipa kwa kupakaa jeli ya aloe vera katika eneo unalosikia maumivu.
31. Hutibu maumivu katika sikio
Matone kadhaa ya aloe vera yakinyunyizwa sikioni yanaweza kuleta nafuu kubwa kama unapatwa na maumivu katika masikio. Hii ni nzuri pia kwa masikio yanayotoa usaha na maumivu mengine katika masikio.
Hapa chini tazama video juu ya namna ya kuandaa jeli ya mshubiri nyumbani kwako na kuinywa kama juisi. Ingawa huyu dada kwenye video analiondoa lile ganda lake la juu lenye rangi ya blue, bado unaweza kuisaga pamoja na maganda yake (isipokuwa ile miiba yake) na bado ikawa nzuri zaidi.
Kama unahitaji aloe vera fresh niachie ujumbe WhatsApp +255766807205

UJUE MLONGE

Mlonge au Moringa oleifera kwa kiingereza umekuwa ukijulikana kama mti wa miujiza kwa karne nyingi katika baadhi ya nchi za Afrika, Asia na katika nchi za Caribbean. Mti huu umeripotiwa kutibu zaidi ya magonjwa 300 ikiwemo magonjwa mbalimbali sugu.
Karibu kila sehemu ya mti huu hutumika kama dawa. Majani ya mlonge yanaweza kutafunwa mabichi, yaliyochemshwa kama mboga au yaliyokaushwa na kusagwa kuwa unga. Unga wa mlonge unaweza kuhifadhiwa kwa miezi kadhaa bila kupoteza ubora na faida zake za kiafya.
Mbegu za mlonge zimekuwa dili kubwa duniani kwa sasa, zinahitajika kwa kiasi kikubwa katika nchi ya Marekani na China na kwa mjibu wa taarifa ni kuwa zinauzwa mpaka shilingi 45000 ya Tanzania kwa gramu 500. Walikuja pia wachina kuzinunua kwa wingi na walipokuwepo hapa Tanzania bei ya mbegu za mlonge ilifika mpaka 11000 kwa kg kwa bei ya jumla yaani kwa anayechukua kg 100 au 500 au 1000 na kwenda juu. Taarifa zisizo rasmi zinadai Wachina hawa walikimbia nchini baada ya serikali kuanza kufuatilia na kuwakamata wakwepaji kodi bandarini. Isingekuwa hivi mpaka leo mlonge ungekuwa umeshatoweka wote Tanzania.
Faida za mlonge zimeandikwa na majarida ya afya na lishe kadhaa duniani. Kile ulikuwa hujuwi ni kuwa viwanda na makampuni mengi ya dawa za hospitalini yamekuwa yakitumia virutubishi vilivyomo kwenye mti huu kutengenezea madawa kwa ajili ya binadamu na wanyama.
MLONGE UNA:
  1. Kalsiamu mara 17 zaidi ya ile ya maziwa ya ng’ombe
  2. Una vitamini C mara 7 zaidi ya ile ipatikanayo katika machungwa
  3. Potasiamu mara 15 zaidi ya ile ya kwenye ndizi
  4. Una vitamini A mara 10 zaidi ya ile ya kwenye karoti
  5. Una protini nyingi mara 9 zaidi ya ile ya kwenye mtindi (Yogurt)
  6. Una Klorofili (kemikali ya rangi ya kijani ipatikanayo katika mimea) mara 4 zaidi ya ile ya kwenye nyasi au majani ya ngano (wheatgrass)
  7. Una madini chuma (iron) mara 25 zaidi ya yale ya kwenye Spinach
  8. Una vitamini A mpaka Z,
  9. Una Omega 3, 6, na 9
  10. Una asidi amino zile mhimu zaidi zinazohitajika na mwili
  11. Una kiasi cha kutosha cha madini ya Zinc ambayo ni madini mhimu katika kuongeza homoni za kiume na nguvu za kiume kwa ujumla

MLONGE NDICHO CHAKULA CHENYE AFYA ZAIDI KULIKO CHAKULA KINGINE CHOCHOTE JUU YA ARDHI;
Mlonge una jumla ya virutubishi 92, mmea au mti mwingine wenye virutubishi vingi baada ya mlonge una virutubishi 28. Mlonge una viondoa sumu 46 na viondoa uvimbe mbalimbali mwilini 36, una asidi amino 18 na asidi amino mhimu zaidi 9 ambazo miili yetu haina uwezo wa kuzitengeneza.
Unga wa majani ya mlonge unao uwezo wa kutibu magonjwa zaidi ya 300 mwilini, magonjwa hayo ni pamoja na;
1. Huko Afrika magharibi madaktari hutumia mlonge kutibu Kisukari
2. Huko India mlonge hutumika kutibu shinikizo la juu la damu
3. Hutibu matatizo au maumivu ya mishipa
4. Hutuliza mapigo ya juu ya moyo (stroke),
5. Hutibu Kansa
6. Pumu
7. Hutuliza wasiwasi
8. Kikohozi
9. Maumivu ya kichwa
10. Inazuia na kushusha lehemu (cholesterol) hata ile ya juu zaidi (hypocholesteremia)
11. Inapunguza mafuta tumboni
12. Inaweka sawa homoni
13. Inatibu maumivu wakati wa hedhi (dysmenorrhea),
14. Unasafisha ini (hepatic detoxification),
15. Unasafisha mkojo na kibofu cha mkojo
16. Unarekebisha matatizo kwenye tezi
17. Unatibu kipindupindu na kuharisha
18. Kifua kikuu
19. Kichwa kizito
20. Uchovu
21. Mzio (aleji)
22. Vidonda vya tumbo
23. Maambukizi kwenye ngozi
24. Maumivu mbalimbali mwilini
25. Huondoa madoa doa meusi kwenye ngozi (blackheads),
26. Husafisha damu,
27. Hutibu matatizo kwenye koo
28. Huondoa makohozi mazito kooni
29. Huondoa taka na msongamano kifuani
30. Hutibu kipindupindu
31. Huondoa mtoto wa jicho au uvimbe kwenye jicho
32. Hutibu maambukizi kwenye macho na kwenye masikio
33. Unatibu homa
34. Maumivu kwenye maungio
35. Huondoa chunusi
36. Hutibu matatizo karibu yote ya ngozi na kinga ya mwili
37. Matatizo kwenye mfumo wa upumuwaji
38. Inatibu Kiseyeye (scurvy)
39. Huongeza uwingi wa mbegu za kiume na nguvu kwa ujumla
40. Unatibu minyoo
41. Huongeza maziwa kwa wingi kwa mama anayenyonyesha
42. Huondoa uvimbe kwenye utumbo mpana (colitis)
43. Unatibu gauti (dropsy),
44. Unatibu kuhara damu (dysentery)
45. Unatibu kisonono ( gonorrhoea)
46. Unatibu tatizo la kukosa usingizi,
47. Unatibu homa ya manjano (jaundice),
48. Unatibu malaria
49. Unatibu U.T.I na matatizo mengine kwenye mfumo wa mkojo
50. Unasidia pia kujenga na kuimarisha misuli
51. Unatibu magonjwa ya mifupa
Mlonge unasafisha mwili wako wote, unasafisha ini, figo, moyo, macho, unaimarisha meno, ngozi na nywele. Wakati unatumia mlonge unakufanya ujisikie vizuri, ujisikie mpya (fresh) na mwenye nguvu. Watu wengi wanaotumia mlonge huwa ni wenye afya nzuri hata kwa muonekano tu hata wanapokuwa na umri mkubwa zaidi ya miaka 90.
Majani ya mti wa mlonge pia yanaweza kutumika kutengeneza biogas (aina ya nishati ya umeme inayotokana na kinyesi cha ng’ombe au takataka). Hutumika pia kama chakula cha wanyama kama sungura, mbuzi, ng’ombe, mbwa nk. Sungura wanaonekana kupenda zaidi mlonge kuliko wanyama wote.
MBEGU ZA MLONGE:
1. Mbegu zake hutumika kama kiuaji sumu na pia hutibu uvimbe. Hutibu maumivu ya kwenye mishipa, baridi yabisi, gauti, kukamaa mishipa, magonjwa ya ngono na majipu. Mbegu hizi hukaangwa kidogo, hupondwapondwa na kuchanganywa na mafuta ya nazi na kupakwa sehemu yenye tatizo.
2. Mbegu za mlonge zilizokaangwa na mafuta yake husaidia watu wanaoshindwa kuzalisha mkojo.
3. Mbegu zake hutumika pia kumtuliza au kumfanya mtu mwenye kifafa a-‘relax’.
4. Mbegu za mti wa Mlonge ni kinga dhidi ya vijidudu (bacteria) wasababishao magonjwa na kuathiri ngozi ikiwemo fangasi.
5. Pia mbegu hutumika katika kusafisha au kuchuja maji ambapo zikipondwa na kuwekwa kwenye maji yenye tope au machafu husababisha uchafu kujikusanya na kuzama chini kisha kuacha maji yakiwa safi na salama kwa kupikia au kunywa badala ya kuchemsha.
6. Mbegu za mlonge pia huongeza kwa kiasi kingi kinga ya mwili (CD4), Kama una tatizo la kinga ya mwili wako kushuka basi tumia mbegu za mlonge kwa mwezi mmoja mpaka mitatu na kinga yako itaimarika sana.
Chukuwa punje 3 na uzimenye ganda lake la juu na utafune mbegu ile ya ndani yote hizo tatu na ukimaliza kuzitafuna kunywa maji ya kawaida siyo ya kwenye friji glasi 2 (nusu lita), fanya hivi kutwa mara tatu.
MLONGE UNATOA WAPI MAAJABU YOTE HAYA?
Matatizo mengi ya kiafya ni matokeo ya lishe yenye viinilishe duni au hafifu jambo linalopelekea kuwa na kinga ya mwili isiyo na nguvu kupigana na magonjwa mbalimbali. Unaporekebisha usawa huo usio sawa wa kinga yako ya mwili kwa kutumia mimea na lishe zingine mhimu za asili hutakawia kuona matokeo mazuri kwenye afya yako.
Uwezo wa mti wa mlonge kuyaweza yote hayo ni kutokana na kuwa na vitamini, madini mbalimbali na viondowaji sumu vingi kuliko mmea mwingine wowote. Wagonjwa wengi wenye UKIMWI katika sehemu nyingi za afrika magharibi wameripoti kuongezeka kiasi kikubwa cha kinga yao ya mwili baada ya kutumia mlonge kiasi cha kutokuhitaji dawa.
NGUVU, UMAKINI, NGOZI YENYE KUPENDEZA, KUTOZEEKA MAPEMA NA KUPUNGUZA UZITO NA UNENE:
Mlonge una viinilishe mhimu vinavyosaidia kuuongezea uwezo mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Vitamini, madini na homoni mhimu zilizomo kwenye mti huu huufanya mwili wako kuwa na usawa unaohitajika kiafya na hivyo kukupa kinga dhidi ya magonjwa mengi bila idadi.
Mlonge una kiinilishe mhimu sana kwa wingi kuliko mmea au mti mwingine wowote duniani mara maelfu kadhaa kiitwacho kwa kitaalamu kama ‘Zeatin’. Zeatin ndiyo hutengeneza seli mpya za ngozi pia huzifanya seli mpya kutengenezwa kwa haraka na kwa wingi zaidi ya zile seli zinazokufa. Hii huleta matokeo mazuri ikiwemo kuondoa mikunjo ya ngozi au ngozi kuzeeka sehemu za uso na sehemu nyingine za mwili na kukupa afya nzuri ya ngozi.
Kwenye mlonge kuna ‘Sulfur’, hii sulfur ni mhimu katika kuunda vitu mhimu kwenye ngozi kama collagen na keratin huku viuaji au viondowaji sumu zaidi ya 30 vinavyopatikana kwenye mlonge ni mhimu kwa ajili ya afya ya ngozi yako.
Mlonge ambao umekuwa ukitumika kwenye vituo vingi vinavyojihusisha na kupunguza uzito huwa una nguvu ya asili ya kupunguza njaa, huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula na kukung’arisha wewe huku ukikuacha na virutubishi vingi mhimu zaidi.
HUIRUDISHA UPYA AFYA YA MWILI WAKO;
Baada ya kufikisha umri wa miaka 30 hivi nguvu zako za mwili huanza kushuka. Mwili wako utaanza kuleta mchonyoto. Utaona unaanza kupoteza umakini nyakati za mchana sababu hukuzingatia nini ule wakati ulipokuwa kijana. Baadhi ya kuharibika kwa afya hakuwezi kurudishwa nyuma ikiwa ni pamoja na kuzorota kwa afya ya meno.
AFYA MBOVU YA MENO INAPELEKEA MAGONJWA KADHAA NA VIFO;
Calcium, Magnesium, Manganese, Potassium, Boron na Vitamini D yote ni madini mhimu ili uwe na meno yenye afya. Magonjwa mengi sugu ni matokeo ya upasuaji wa kwenye kinywa. Kila mtu anapaswa kulinda afya ya meno yake kuanzia leo kwani meno yakishaoza au kuharibika huwa ni vigumu kupona na kurudi kwenye hali yake ya mwanzo. Afya ya meno yako itaamua ni miaka mingapi unaweza kuishi.
Kila mmoja wetu anatakiwa kutimiza wajibu wake linapokuja suala la afya ya mwili wako. Tumia google tafuta taarifa za kile unachokula au kunywa kila siku. Kichwa kitakuuma utakapojua ni nini unakula!. Nenda YouTube angalia video hizi: “Food Matters” na “Dying to have know”. Tafuta kwenye chaneli ya Discovery movie inaitwa “Moringa The Miracle Tree” na video nyingine inaitwa ‘Moringa Oleifera’.
BIDHAA NYINGI ZA AFYA HAZINA AFYA YOYOTE;
Bidhaa nyingi za afya hazina utafiti halisi (genuine) unaojitegemea au zina maelezo kutoka kwa mtengenezaji tu wa hiyo bidhaa. Mlonge una mfululizo wa tafiti za watu wengi na shuhuda za watu kote duniani zaidi ya miaka 4000 iliyopita. Ni mtishamba kwa asilimia 100 unaoota wenyewe.
Matumizi ya mlonge kama kiua vijasumu (antibiotic) kwenye tiba asili yalianza miaka maelefu iliyopita. Mlonge ulitumika kwa mara ya kwanza kama dawa zaidi ya miaka 2000 kabla ya Kristo. Watabibu wazamani wa Misri na Ugiriki waliona faida nyingi za mti huu na wakautambulisha kwa Warumi na baadaye mlonge ukaenea mashariki mwa India na sehemu ya chini ya nchi ya Uchina, kusini mashariki mwa Asia na Ufilipino na magharibi mwa Misri kuzunguka mediterania na mwishowe ukafika kwa Wahindi mashariki mwa Amerika. Leo zaidi ya watu milioni 400 wanatumia mlonge. Shirika la afya duniani (W.H.O) limekuwa likitumia mlonge zaidi ya miaka 40 sasa.
Unga wa majani ya mlonge unapaswa uwe ni wa kijani kweli kweli na majani yake yawe yalianikwa kivulini na siyo juani. Anza na kijiko kidogo kimoja ukichanganya na vimiminika kama maji ya uvuguvugu au juisi yoyote ya matunda uliyotengeneza mwenyewe nyumbani kutwa mara moja na taratibu ongeza kiasi cha dawa kadri unavyohitaji. Unaweza kuuchanganya pia kwenye wali wakati unakula au unaweza kuweka ndani ya kikombe cha uji au unaweza kutumia kama majani yako ya chai ingawa hautakiwi uchemshe sana kwenye moto.
Mti wa mlonge sasa umeanza kuwa maarufu huko Marekani hii ni kutokana na mti wenyewe kuendelea kupata umaarufu miongoni mwa watu wanaojali afya zao. Ingia google andika ‘Moringa plants for sale’ utagundua keyword hiyo inatafutwa kila siku mara maelfu. Watu wengi pia wameanza kilimo cha mlonge kama biashara ya kuwaingizia kipato. Ukiwa na miti 200 tu ya mlonge shambani kwako tayari wewe siyo mwenzetu.
Mti wa mlonge ni moja ya miti mhimu katika sehemu yote ya dunia. Kadri watu wanavyoendelea kuutafiti na kuusoma mti huu ndivyo mahitaji ya unga wa majani yake, mbegu zake, unga wa mbegu zake na mafuta ya mbegu zake yatakavyozidi kuongezeka na kuongezeka.
Utahitaji mlonge? Niachie tu ujumbe WhatsApp +255766807205.